Thursday, April 22, 2010

Timeless quotes

For this post, Id like to share some quotes I found interesting and otherwise worthy to learn, keep and share. I think they make not only for great readings but are nuggets worth modeling life against. What do you think?

1. When things go wrong as they sometimes will, When the road you're trudging seems all up hill, When the funds are low and the debts are high, And you want to smile, but you have to sigh, When care is pressing you down a bit, Rest if you must, but don't you quit. Life is queer with its twists and turns, As every one of us sometimes learns, And many a failure turns about, When he might have won had he stuck it out. Don't give up though the pace seems slow--You may succeed with another blow, Success is failure turned inside out--The silver tint of the clouds of doubt, And you never can tell how close you are, It may be near when it seems so far; So stick to the fight when you're hardest hit--It's when things seem worst that you must not quit. (Unknown)

2.Our deepest fear is not that we are inadequate. Our deepest fear is that we are powerful beyond measure. It is our light, not our darkness, that most frightens us. Your playing small does not serve the world. There is nothing enlightened about shrinking so that other people won't feel insecure around you. We are all meant to shine as children do. It's not just in some of us; it is in everyone. And as we let our own lights shine, we unconsciously give other people permission to do the same. As we are liberated from our own fear, our presence automatically liberates others.
(Nelson Mandela)

3.Yesterday is history. Tommorrow is a mystery. And today? Today is a gift that's why they call it the present.
(Unknown)

4. ...the way I see it, you can either run from it, or learn from it. - The Lion King
(Rafikki)

5. Never be afraid to try, remember...Amateurs built the ark, Professionals built the Titanic.(Unknown) - one of my very favourites

6.One grain may tip the scale. One man may make the difference between victory and defeat.(Mulan)

I could go on and on, lets muse on these!

Monday, March 8, 2010

Thursday, February 11, 2010

Climate change

So I joined this youth network: AYICC. As you can guess, it deals with climate change and not just its change as the new catch word, climate change is a grim reality that must be faced simply because it is here with us. AYICC is The Africa Youth Innitiative on Climate Change, Kenyan chapter.

Saturday 13th Feb, Emerging Leaders Summit, this event will take perspective on our generations challenge still on climate change. This inagaural event will see youth engage leaders in Kenyan society (not restrictive to these alone- feature will see an ambassedour open the sessions) for a whole day. Chief co-ordinator AYICC will be presenting a sessional paper and resolutions on behalf.

In being concious of my environment, I hope to make a change and change the tide of climate and its effects in a positive direction. Go AYICC...

Wednesday, June 3, 2009

Mwerevu huling'amua

Fumbo mfumbie mjinga.

Mawazo yangu ya karibuni yanielekeza siku za usoni. Angalau jana kashakwenda sirudi, ganda la muwa la jana chungu kaona kivuno.

Mara kwa mara nimesikia ya kwamba ukitaka kutabiri ya kesho, tazama jana. Pinda shingo utazame yaliyokwisha tendeka na kwayo, utapata maono yasiyopatikana pengine popote. Kwa muda uliosalia, tafakari ya kuwa:

1. Kupotea njia ndiko kujua njia

2. Hiari yashinda utumwa

3. Kila chombo kwa wimbile


Hapana kitu cha fahari tulichonacho waja ila muda. Ni bora tufahamu njia na nia, na MUDA wake.

Monday, April 13, 2009

Havitatajwa fedhaluka wala bilauri

Hakika kuna shimo wachimbako fedha, na mahali wapatapo dhahabu waisafishayo. Chuma hufunikwa katika ardhi,na shaba huyeyushwa katika mawe. Binadamu hukomesha giza;huyatafutatafuta hata mpaka ulio mbali, mawe ya giza kuu, giza tupu.

Hufikia shimo mbali na makao ya watu; palikosahaulika na nyayo zipitazo. Hining'inia mbali na watu, huyumba-yumba huko na huko. Katika ardhi ndimo kitokeamo chakula; na chini yake hupinduliwa kama kwa moto. Mawe yake ni mahali zipatikanapo yakuti; nayo ina mchanga wa dhahabu.

Njia ile hapana ndege mkali aijuaye, wala jicho la tai halijaiona. Wanyama wakali wajivunao hawajaikanyaga, wala simba mkali hajaipita. Huunyoshea mwamba wa gume gume mkono wake, huipindua milima hata misingi yake. Hukata mifereji kati ya majabali,Na jicho Lake huona kila kitu cha thamani. Hufunga vijito visichuruzike; na kitu kilichostirika hukifunua.

Bali hekima itapatikana wapi, mahali pa ufahamu ni wapi?

Mwanadamu hajui thamani yake, wala haionekani katika nchi ya walio hai.

Vilindi vyasema, "Haimo ndani yangu"
Na bahari yasema, "Haiko kwangu"

Haipatikani kwa dhahabu, wala fedha haitapimwa iwe thamani yake. Haiwezi kutiwa thamani kwa dhahabu ya Ofiri. Wala kwa shohamu ya thamani nyingi, wala kwa yakuti ya samawi.

Dhahabu na vioo haiwezi kulinganishwa nayo; wala kubadili kwake hakutakuwa kwa vyombo vya dhahabu safi. Havitatajwa fedhaluka wala bilauri; Naam Kima cha hekima chapita marijani. Yakuti ya rangi ya manjano ya kushi haitasawazishwa nayo, wala haitatiwa kima kwa dhahabu safi.

Basi hekima yatoka wapi? kwa kuwa imefichwa mbali na macho ya wote walio hai, na kusitirika na ndege wa angani. Uharibifu na mauti husema, "tumesikia habari zake kwa masikio yetu."

Mungu ndiye aijuaye njia yake, Naye ajua mahali pake. Maana anatazama hata miisho ya nchi, na kuona chini ya mbingu nzima. Apate kuufanyia upepo uzito wake; naam anayepima maji kwa kipimo. Hapo alipoiwekea mvua amri, na njia kwa umeme wa radi. Ndipo alipoiona na kuitangaza; aliidhibitisha, naam na kuichunguza.

Kisha, akamwambia mwanadamu: Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima. Na kujitenga na uovu ndio ufahamu

Saturday, March 28, 2009

Mkenya Mzalendo

Naishi, natumaini
Najitolea daima Kenya, Hakika ya bendera
Ni udhabiti wangu, Nyeusi ya wananchi na
Nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
daima mimi mkenya, mwananchi mzalendo

Maneno haya si utenzi wangu mimi. Ni mwimbaji Eric Wainaina.

Nimekinai wimbo mwenyewe; kwani hadi sasa, hamna msanii mwingine ambaye ametupa kazi au wimbo ambao ni wa kizalendo na tena wenye kufikia kiwango cha kimataifa. Wimbo ambao ni wa kuburudisha na vilevile wenye ujumbe dhabiti - unaozungumzia wajibu wetu kama wananchi.

Mara ya kwanza kuusikia wimbo mwenyewe si juzi, la. Niliusikia miaka rudi - nikiwa shule ya upili papa hapa jijini nairobi. Kama wanakwaya shuleni, tulialikwa sherehe ya kutamatisha kibarua cha kukusanya mihela ambayou ingewaendea watoto waathiriwa kupunguza njaa humu nchini. Tulishinda njaa mchana kutwa na hela kiwango cha chakula cha mchana tukazikusanya. Tuliwapa wahisani tukitumaini na pia kuwaamini wazifikishe tulikokusudia.

Jioni baada ya haya yote, kijana mmoja ambaye wakati huo alikuwa akianzilia ulimwengu wa sanaa na uimbaji alikwea jukwaa. Kimya kilitanda mithili ya gubi gubi ya blankenti nzito alipoanza kuutirisha wimbo huu. Aliuimba kwa lugha ya kimombo na kwa kweli ungalilinganisha muziki wenyewe na mwingine wetu wakati huo, haungeamini ni utunzi na uimbaji wa mzaliwa.

Nisipoteze mada; wakenya lazima tuanze kujivunie ukwasi wetu wa lugha, wa utamaduni, wa manthari ya nchi, wa utaratibu wetu. Tusimame tisti, na kujivunia hali ii hii tuliyonayo. Tujivunie Kenya na Ukenya.

Video yenyewe: http://www.youtube.com/watch?v=TTzgA4t2Da0&feature=related